Abstract Wikipedia:Kuhusu
Abstract Wikipedia ni nini?
Abstract Wikipedia ni mradi mpya ndugu wa Wikipedia.
Maono ya Wikipedia ni ulimwengu ambao kila mtu ana ufikiaji wa jumla ya maarifa yote. Abstract Wikipedia itasaidia jumuiya ya wanaojitolea kuchangia Wikipedia na miradi inayohusiana nayo kuziba mapengo ya maarifa kwa ufanisi zaidi.
Wikipedia ina makala kuhusu zaidi ya mada milioni 20 katika lugha zaidi ya 300. Lakini hakuna hata moja ya lugha hizi inayoweza peke yake kutoa ufikiaji wa maarifa kuhusu mada hizi zote milioni 20: Kiingereza kina zaidi ya makala milioni saba, Kikroeshia kina 230,000, na Kiswahili kina 100,000. Isipokuwa kama unazungumza lugha hizo, maarifa hayo hayapatikani kwa urahisi kwako. Na ingawa tafsiri za mashine zimeboreshwa sana kutokana na maendeleo ya hivi karibuni katika AI, bado hazijafikia kiwango cha kutoa tafsiri unazoweza kuziamini kwa jozi nyingi za lugha.
Abstract Wikipedia hufanya hivyo bila kutegemea AI. Kila hatua hubaki chini ya udhibiti wa binadamu, na inapatikana na inaweza kuhaririwa na wachangiaji wa kujitolea. Hakuna “mauzauza”, wala makosa yasiyoeleweka au yasiyoweza kurekebishwa: Ikiwa kuna kosa lolote, kulirekebisha ni hatua moja tu, na kuna uwazi kamili kuhusu jinsi maandishi yalivyoundwa. Si tu modeli ya uwezekano inayochagua mji mkuu wa Kenya kwa kubahatisha kila mara. Ni maarifa yaliyopangwa na kusimamiwa na binadamu.
Abstract Wikipedia inafanyaje kazi?
Makala katika Abstract Wikipedia zinahifadhiwa katika mfumo ambao hautegemei lugha za binadamu. Kiolesura cha Abstract Wikipedia kinawaruhusu wachangiaji wa kujitolea kuunda na kusimamia mfumo huo usiotegemea lugha. Katika hatua ya pili, mfumo huo unabadilishwa kuwa maandishi ya lugha ya binadamu. Hatua zinazohitajika ili kufanikisha hili pia zinaundwa na kusimamiwa na jumuiya ya wajitoleaji kupitia Wikifunctions. Hatua hizi zinaweza kutumia data zilizopo kwenye Wikidata, kama vile kutafuta idadi ya watu, tarehe za kuzaliwa, au miundo ya kisarufi isiyo ya kawaida, ambayo imeongezwa na inasimamiwa kwenye Wikidata na jumuiya za wajitoleaji.
Tazama Help:How to create an article kwa mwongozo wa hatua kwa hatua.
Hebu tufuate mfano mmoja: Nigeria ndiyo nchi yenye watu wengi zaidi barani Afrika. Katika Abstract Wikipedia, hili linaweza kuhifadhiwa kama:
Au, kama tutatumia lebo za Kiingereza kwa vitambulishi hivi:
Hii ni wito (call) wa kazi (function) kwenye Wikifunctions. Kulingana na lugha, kazi nyingine inaitwa. Kwa Kiingereza, tunapata wito ufuatao wa kazi:
Na hilo husababisha kupata maandishi ya Kiingereza yafuatayo:
Kama tungelichagua Kijerumani, kazi nyingine ingetumika (kuitwa):
Na hilo kwa upande wake lingetoa maandishi yafuatayo ya Kijerumani:
Mfano wenye lugha zaidi unaweza kupatikana hapa.
Abstract Wikipedia huwaleta pamoja jamii nyingi kutoka Harakati ya Wikimedia na huwawezesha kufanya kazi kwa pamoja. Data ya msingi ya msamiati na data iliyopangwa kuhusu mada nyingi kutoka Wikidata, kazi (functions) zinazobeba hesabu na michakato muhimu kutoka Wikifunctions, pamoja na picha na ramani kutoka Wikimedia Commons, vyote hivi huunganishwa katika Abstract Wikipedia na kuwekwa wazi kwa ajili ya matoleo zaidi ya 300 ya lugha za Wikipedia.
Lengo la Abstract Wikipedia ni kufanya maarifa zaidi yapatikane kwa watu zaidi katika lugha zaidi, na kuwawezesha wahariri wa kujitolea kuwa na ufanisi zaidi na kufanya kazi katika lugha tofauti, bila kujali lugha wanazozungumza. Maboresho ya maarifa yataenezwa moja kwa moja hadi Wikipedia zote, makosa yataonekana haraka zaidi na kurekebishwa kwa ufanisi zaidi, na ushirikiano kati ya lugha tofauti utawezekana. Tunavunja vizuizi vya lugha vinavyotenganisha maarifa.